• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Makamu wa Rais Azindua Mkakati wa Kudhibiti Upotevu wa Mazao

Posted on: August 1st, 2019

Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Agosti Mosi, 2019 amezindua mkakati wa udhibiti wa upotevu wa mazao wenye lengo la kumsaidia mkulima namna ya utunzaji Bora wa mazao baada ya mavuno.

 

Mama Samia amezindua mkakati huo katika ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Nane Name Kitaifa, uliofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki  katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Amesema upotevu wa mazao ni moja ya changamoto zinazowakabili wakulima na kupelekea kuwa na tija ndogo huku akizitaja changamoto nyingine kuwa ni matumizi hafifu ya mbolea,  kutopata mbegu na viuatilifu kwa wakati na vilivyo bora na kutotumia kanuni bora za kilimo.

Aidha, Mhe. Makamu wa Rais ametoa wito kwa Taasisi za Umma, binafsi, vyama vya ushirika na Taasisi za kiraia zinzojishughulisha na Maendeleo ya Kilimo kuhakikisha wanarekebisha kosoro zilizopo na kutoa elimu bora na kutosha inayojibu changamoto hizo.

Katika hatua nyingine Mhe. Makamu wa Rais ametoa rai kwa watafiti wote nchini kutoa matokeo ya tafiti zao kwa maafisa ugani na wadau wengine ili wakulima wanufaike na matokeo hayo.

Akizungumzia mkakati wa kudhibiti upotevu wa mazao miaka 10, Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga amesema lengo la serikali ni kuhakikisha inapunguza upotevu wa mazao kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2025.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya mikoa inayounda Kanda ya Nanenane ya Ziwa Mashariki ni kuvifanya viwanja vya maonesho ya Nanenane Nyakabindi kuwa ni mahali patakapojibu kwa vitendo sera za wizara ya kilimo na pawe mfano kwa wananchi kujifunza Kilimo Biashara.

Pia ametoa wito kwa wanunuzi wa pamba kuendelea kununua pamba kwa bei elekezi ya shilingi 1200 na taasisi za fedha kutoa fedha kwa wanunuzi pamba ya wakulima inunuliwe, huku akiiomba Serikali kuridhia sehemu ya fedha ikakatwa fedha hiyo iweze kuwekeza kwenye ujenzi wa kiwanda cha nguo kwa kushirikiana na wadau wengine ili kuwa na soko la uhakika la pamba.

Mkoa wa Simiyu uko tayari kutekeleza agenda ya ujenzi wa kiwanda cha nguo  kupitia Vyama vya Ushirika vya Msingi, Chama Kikuu cha Ushirika (SIMCU) na wawekezaji walio ndani ya mkoa huku akibainisha kuwa

Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanafanyika kwa mara ya pili mfululizo sasa katika Kanda ya Ziwa Mashariki inayoundwa na Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga, yakiwa na Kauli Mbiu isemayo Kilimo, Mfugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/08/makamu-wa-rais-azindua-mkakati-wa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa