Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi wa Wilayani ya Busega kutokaa na fedha majumbani badala yake watumie Taasisi za kifedha kutunza fedha zao kwa ustawi wa maisha yao na Usalama wa Fedha zao.
Mhe. Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua tawi la NMB Nyashimo wilayani Busega Machi 06, 2020 ambapo ameipongeza benki huyo kusogeza huduma karibu na wananchi.
"Wilaya hii ya Busega na Mkoa wa Simiyu kwa ujumla una uchumi mkubwa, mna uchumi utokanao na ziwa yaani uvuvi, uchumi wa mifugo, uchumi wa kilimo; hivyo sikae na fedha mikononi pelekeni benki ili benki itumie kwa maendeleo yetu na ya kwako binafsi," alisema Mhe. Makamu wa Rais.
Katika hatua nyingine Mhe. Makamu wa Rais ameipongeza Benki ya NMB kwa kuanzisha huduma za bima na huduma maalum kwa ajili ya kundi la waendesha pikipiki (bodaboda) na kubainisha kuwa huduma hiyo umechangia kuwapunguzia hali ya kubaki na fedha mfukoni na kuwapunguzia haki ya kuendelea kuwashawishi wanafunzi wa kike na kuwalaghai na wakati mwingine kuwapa ujauzito.
Naye Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Ashatu Kijaji ameagiza Benki Kuu ya Tanzania kukaa na benki nyingine nchini ili kujadili namna ya kupunguza riba kwa wakopaji(wananchi) kwa kuwa Serikali imezipunguzia benki hizo riba katika mitaji ya kuendeshea benki hizo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameishukuru Benki ya NMB kwa namna ambavyo imekuwa ikichangia katika maendeleo ya Mkoa wa Simiyu ambapo hadi sasa imechangi shilingi milioni 200 katika sekta ya Elimu.
MWISHO
Bariadi - Somanda
Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.
Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054
Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054
Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz
Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa