• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Kamati ya Olimpiki Tanzania yatoa Mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo mkoani Simiyu

Posted on: August 14th, 2017

Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC) imeanza kutoa mafunzo ya siku tano ya Utawala na Uongozi wa Michezo Mkoani Simiyu, ambayo yamelenga kuleta tija katika kusimamia na kuendeleza Michezo.

Mafunzo hayo yanawahusisha Maafisa Michezo Mkoa na Wilaya, Viongozi wa Vyama mbalimbali vya Michezo  na walimu wa michezo kutoka katika baadhi ya shule za msingi na sekondari mkoani Simiyu.

Mkurugenzi Mkuu wa Mafunzo hayo Ndg.Suleiman Jabir amesema lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwasaidia Maafisa Michezo, viongozi wa vyama vya michezo ngazi ya mkoa na wilaya sambamba na walimu wa michezo kupata mafunzo ya kiufundi katika kusimamia na kuendeleza michezo, ambayo hutolewa katika mikoa yote hapa nchini, chini ya usimamizi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC).

Akizungumzia ushiriki wa wanawake Ndg. Jabir amesema Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) imehakikisha kuwa wanawake wanashiriki kwa asilimia 40 katika mafunzo hayo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa la mwaka 2016 la kuwashirikisha wanawake katika masuala muhimu ya kimichezo ikiwemo suala la uongozi.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi amesema, Utawala na uongozi wa michezo ulio bora ni msingi wa kuongoza na kuendeleza michezo  kwa mujibu wa sheria,kanuni na taratibu.

“Kamati ya Olimpiki imeandaa mafunzo haya kwa wakati muafaka kwa sababu wanahitajika viongozi wenye taaluma ya kisasa ya namna ya kuongoza michezo na wanamichezo,ambao watakwenda na wakati kutenda kazi zao bila mgongano au vurugu “ amesema Kilangi.

Kilangi amewataka washiriki kuhakikisha kuwa wanazingatia mafunzo watakayopata na kuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao, ili mafunzo hayo yasiishie tu katika Taasisi walizopo bali elimu hiyo ifike hadi ngazi ya vijiji ambako ndiko kwenye wachezaji wengi.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ametoa wito kwa washiriki kutumia mafunzo hayo kama chachu katika kufuata taratibu zote za uendeshaji wa vilabu na vyama vya michezo katika mkoa wa Simiyu ikiwa ni pamoja na kufuata katiba.

Ameongeza kuwa pamoja na kuchukulia michezo kama burudani na sehemu ya kuimarisha afya, washiriki hao wanapaswa kuwasaidia wachezaji kutumia michezo kama ajira inayoweza kuwaingizia kipato.

Kwa upande wake Afisa Michezo wa Mkoa, Ndg.Anthony Komba amesema mafunzo hayo yatawasaidia washiriki kusimamia michezo kwa weledi mkubwa, kuibua vipaji na pia yatasaidia vyama vya michezo kusimamia vema vyama vyao, ikiwa ni pamoja na kufuata katiba hali itakayowasaidia kuepuka migogoro katika vyama.

Mafunzo kwa Maafisa Michezo, viongozi wa vyama vya michezo Mkoa na Wilaya pamoja na walimu wa michezo kutoka katika baadhi ya shule za msingi na sekondari Mkoani Simiyu, ambayo yamefunguliwa rasmi leo, yanafanyika katika ukumbi wa BARIDECO mjini Bariadi na yatahitimishwa siku ya Ijumaa tarehe 18/08/2017.


Baadhi ya washiriki wa Mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo yaliyoandaliwa na Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC) wakifuatilia Hotuba ya Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi(hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo hayo kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka mjini Bariadi.

Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi(wa tatu kulia walioketi) katika picha ya pamoja na maafisa michezo, viongozi wa vyama vya michezo na walimu wa michezo wa Mkoa wa Simiyu, wanaoshiriki wa Mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo mjini Bariadi ambayo yameandaliwa na Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC); (wa pili kulia) Mkurugenzi Mkuu wa Mafunzo Ndg.Suleiman Jabir


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa