• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Aiomba Serikali kutoa Kipaumbele Ujenzi wa Uwanja wa Ndege Simiyu

Posted on: February 17th, 2018

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka wa Viwanja vya Ndege nchini (TAA),  Richard Mayongela ameiomba serikali kutoa kiupaumbele cha ujenzi wa Viwanja vya Ndege kwa mikoa ya Simiyu na Lindi katika bajeti ya mwaka 2018/2019 ili kuongeza fursa za uwekezaji na utalii.

Mayongele ametoa ombi hilo leo katika kijiji cha IGEGU kata ya Sapiwi wilayani  BARIADI katika eneo linalotarajiwa kujengwa Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Simiyu, wakati wa ziara ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  Prof. Makame Mbarawa mkoani Simiyu.

Amesema hatua za awali za maandalizi ya ujenzi wa Uwanja huo zimekamilika ambapo usanifu na upembuzi yakinifu vimeshafanyika na makadirio ya awali yanaonesha kuwa mradi huo utagharimu takribani shilingi bilioni 95.56 na utakapokamilika utawezesha ndege zenye uwezo wa kubeba  kuanzia watu 75 na kuendelea kutua.

Ameongeza kuwa Ujenzi wa Uwanja huo utakapokamilika utakuwa ni chachu ya maendeleo kwa Mkoa huo katika nyanja za uchumi na utalii  na utachangia kuufungua mkoa wa Simiyu kiuchumi pamoja na mikoa mingine ya kanda ya Ziwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema kukamilika kwa Uwanja huo itakuwa ni faida kubwa kwa kuwa utakuwa  Uwanja pekee wa Serikali hapa nchini ambao Watalii watautumia kuifikia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa urahisi kuliko viwanja vingine.

“Tunajenga Uwanja ambao kimkakati unakaa mpakani mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, karibu na uwanja huu kuna hii barabara ya inayotunganisha na Mkoa wa Shinyanga kupitia Malampaka ambako kutajengwa Reli ya Kisasa, hapa jirani  tuna eneo ambalo tutajenga Kiwanda cha Vifaa tiba, mbele yeke tunaanzisha Kanda ya Nanenane ...tunaamini kukamilika kwa mradi huu kutakuwa na faida sana  kwa Serikali na wananchi”  alisema Mtaka

Waziri wa Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amewahikikishia viongozi wa Mkoa wa Simiyu juu ya ujenzi wa uwanja wa ndege Simiyu, lakini akatoa angalizo kuwa wakati kufanya tathmini ya fidia ya eneo la ujenzi,  gharama ya fidia  isiwe kubwa vinginevyo Uwanja huo hautaweza kujengwa.

“Wale watakaokuja kufanya tathmini wahakikishe gharama ya fidia inakuwa chini sana na ifanywe kwa mujibu wa sheria, hatutaweza kuwadhulumu watu lakini tuhakikishe tathmini inafanyika kwa mujibu wa sheria” alisisitiza Waziri Mbarawa.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji cha Igegu mahali unapotarajiwa kujengwa uwanja huo, Diwani wa Kata ya Sapiwi, Mhe.Kibuga Gamalieli amesema wananchi wanasubiria kwa shauku kubwa kuona Uwanja huo unakamilika na akamuhakikishia  Waziri Mbarawa kuwa wananchi hawatadai fidia kubwa katika eneo hilo kwa kuwa wanataka maendeleo.

Waziri Mbarawa yuko Mkoani Simiyu kwa ziara ya siku mbili ambapo leo pamoja na kutembelea eneo la ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mkoa Simiyu amezungumza na watumishi wa Taasisi zote zilizo chini ya Wizara yake, amekagua Ujenzi wa Hospitali ya Mkoa na Nyumba za Viongozi wa Mkoa  na kutembelea Kambi ya Mkandarasi wa Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Bariadi-Maswa kata ya Luguru wilayani Itilima

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:https://simiyuregion.blogspot.com/2018/02/kaimu-mkurugenzi-wa-viwanja-vya-ndege.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa