• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

JKT Yajipanga Kufundisha Wananchi Teknolojia za Ufugaji Samaki Maonesho Ya Nanenane Simiyu

Posted on: July 28th, 2018

Naibu  Mkurugenzi  Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa(SUMA JKT),  Luteni Kanali Peter Lushika  amesema  JKT  limedhamiria kuwafundisha wananchi watakaofika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Bariadi  Mkoani Simiyu, teknolojia mbalimbali za ufugaji wa samaki ikiwa ni pamoja na ufugaji kwa kutumia mabwawa, matenki  na vizimba(ndani ya ziwa), ili kuwa na uhakika wa upatikanaji wa samaki na kuzuia uvuvi haramu.

Luteni Kanali Lushika ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya hali ya maandalizi ya Jeshi hilo katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018  na namna walivyojipanga kutoa elimu wa wananchi katika maeneo mbalimbali hususani katika kilimo, ufugaji na uvuvi.

“Tunajua wengi wanafahamu ufugaji wa samaki kwenye mabwawa, mwaka huu tunawaletea teknolojia ya ufugaji wa samaki kwenye matenki, walioko ziwani tutaonesha ufugaji wa samaki kwenye vizimba, teknojia hizi zitamsaidia mvuvi kuvua kuwa na uhakika wa upatiakanaji wasamaki, uhifadhi wa mazingira na kuondokana na uvuvi haramu” alisema Luteni Kanali Lushika.

Amesema JKT itawaeleza wananchi kuwa ufugaji wa samaki ni njia pekee ya kumwezesha mvuvi kupata samaki wakati wowote atakaohitaji hasa ufugaji  kwa kutumia  matenki.

Ameongeza kuwa pamoja na kuona teknolojia hizo  JKT itaandaa madarasa katika uwanja wa nanenane kwa ajili ya kufundisha wakulima, wafugaji, wavuvi, wajasiriamali ili waweze kuona mbinu za kilimo, ufugaji na uvuvi bora na matumizi bora ya pembejeo.

Katika hatua nyingine Luteni Kanali Lushika amesema ili kufikia Tanzania ya Viwanda lina mpango wa kuanzisha kiwanda cha kuchakata pamba ambacho kitachakata pamba kutoka ikiwa ghafi mpaka kufikia kwenye zao la mwisho ambalo ni nguo, hivyo kitaliongezea zaidi thamani zao la pamba.

Naye Luteni Joseph Lyakurya Meneja wa Mradi Sumaponics amesema teknojia ya kufuga samaki kwa kutumia matenki ni nzuri kwa kuwa inatumia eneo dogo la ardhi , maji kidogo lakini inakuwa na uwezo wa kuchukua samaki wengi ikilinganishwa na teknolojia ya mabwawa, hivyo akatoa wito watu wafike Uwanja wa Nanenane wajifunze.

Kwa upande wao Vijana wa JKT wamesema mafunzo waliyoyapata katika teknolojia mbalimbali yamewawezesha kupata maarifa ambayo yanaweza kuwasaidia kujiajiri wenyewe,  hivyo wakatoa wito kwa wananchi kwenda kuona teknolojia hizo.

“Kama mtaalam  wa masuala ya uvuvi niliyehitimu chuo cha uvuvi Kigoma, nikiwa JKT nimepata elimu ya vitendo zaidi ya kile nilichokipata chuoni, tukiwa hapa Nanenane Bariadi  tutatoa elimu kuhusiana na masuala ya uvuvi kwa kutumia vizimba, nawaomba wananchi waje wajifunze, maana ufugaji wa samaki nao una tija katika Tanzania ya Viwanda” alisema Almasi Idd Yusuph kikosi cha 822 Lwamkoma JKT.

“Miimi nikiwa JKT nimejifunza namna ya kuandaa bustani kutokana na mafunzo niliyopata naweza kutambua  udongo mzuri na ambao  si rafiki kwa kilimo cha bustani kama huu, kupitia maonesho haya wananchi wataelewa ni namna gani wanaweza wakaufanya udongo huu ukafaa na wakalima bustani” alisema Nasri Mataka Kijana wa JKT 822 KK Lwamkoma Mara.

Naye Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa SUMA JKT Meja Peter Sebyiga amesema JKT inatoa huduma na kuzalisha bidhaa mbalimbali kwa kuzingatia ubora , muda unaokubalika na jamii kwa bei rafiki kwa wateja, hivyo akatoa wito kwa wananchi kufika kwenye maonesho ya Nanenane ili kuona bidhaa hizo kutoka kwenye viwanda, kilimo, mifugo na uvuvi.

Meja Sebyiga ametoa wito kwa Taasisi, Makampuni na watu binafsi kutumia samani zinazotengenezwa na Kiwanda cha Jeshi la Kujenga Taifa kwa ajili ya matumizi ya Ofisi na nyumbani na kusisitiza kuona umuhimu wa Watanzania kupenda vya kwao.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/07/jkt-yajipanga-kufundisha-teknolojia-za.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa