• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Halmashauri Zatakiwa Kukamilisha Utoaji wa Vitambulisho kwa Wazee Kufikia Juni 2021

Posted on: December 5th, 2020

Rai imetolewa kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani Simiyu kuhakikisha kuwa wanakamilisha zoezi la utoaji wa vitambulisho vya matibabu kwa wazee kufikia mwezi Juni 2021, ili wazee waweze kupata huduma za matibabu katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya kama Serikali ilivyodhamiria.

Rai hiyo imetolewa Novemba 5, 2020 Mjini Bariadi na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka katika uzinduzi wa Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Simiyu..

“Mkoa kupitia Halmashauri umefanya utambuzi wa jumla ya wazee 68,175 kwa lengo la kuhakikisha kuwa wanapatiwa huduma muhimu, hadi sasa  jumla ya mabaraza 770  ya wazee yameundwa katika ngazi zote ; kuhusu upatikanaji wa vitambulisho vya matibabu bure, jumla ya wazee 18, 911 wamepatiwa vitambulisho hivyo ndani ya mkoa sawa na asilimia 28,’ alisema Kiswaga.

Mabaraza si ya kiitikadi hivyo kila mtu mwenye umri wa miaka sitini na kuendelea ana haki ya kujiunga na kuwa mjumbe wa Baraza la Wazee mahali alipo, huku akiahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Wazee na kukukutana na wazee mara kwa mara ili kuhakikisha kuwa inawasilikiza na mahitaji yao muhimu yanapatikana.

Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa, Bibi.Mwanahamisi Kawega amesema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itahakikisha inasimamia utekelezaji wa suala la ugawaji wa vitambulisho vya matibabu kwa wazee katika Halmashauri zote ili wazee wote waweze kuvipata kwa wakati.

Aidha Kawega ameongeza kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu itawaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri kuwaalika viongozi wa mabaraza ya wazee kualikwa katika mabaraza ya madiwani ili waweze kuwasilisha kero zao na kupatiwa ufumbuzi.

aye Meneja Mradi kutoka Shirika la NABROHO SOCIETY FOR THE AGED linalojihusisha na utetezi wa haki za wazee , Bw. Kubini Nkondo ameipongeza Serikali kwa namna inavyotoa kipaumbele kwa wazee na namna ilivyokomesha mauaji ya wazee.

"Wazee wamepitia changamoto nyingi ukizungumzia hata suala la mauaji ya wazee, takwimu awali zilikuwa juu sana lakini katika utawala huu tunazungumzia mauaji hayo kupungua mpaka kufikia 'digit' (tarakimu) moja, Mkoa wa Simiyu ambao ulikuwa ukitajwa katika Mkoa 10 inayoongoza kwa mauaji ya wazee sasa hivi haitajwi hata tena katika mikoa inayoongoza kwa mauaji hayo," alisema Nkondo.

Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Mkoa wa Simiyu, Bw. Lameck Sendo amesema Baraza hilo litaendelea kushirikiana na Serikali katika kushughulikia haki mbalimbali za wazee huku akiomba Serikali kuitungia sheria Sera ya wazee ya mwaka 2003 ili iweze kutumika katika kuwaongoza pamoja na miongozo iliyopo.

Afisa Ustawi wa Jamii Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bw. Daniel Mapunda amesema Mkoa wa Simiyu una takribani wazee 68,175, hivyo kwa mujibu wa Sera ya Wazee ya mwaka 2003 Baraza la Wazee la Mkoa litakuwa ni chombo maalum cha kuwasemea wazee na kushiriki katika maeneo mbalimbali ya kimaamuzi.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/12/halmashauri-zatakiwa-kukamilisha-utoaji.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa