Jumla ya vikundi 16 vya wanawake na vijana vilivyopo katika kata 36 Wilayani Maswa Mkoani Simiyu vimepatiwa mkopo wa shilingi Milioni 50 kwa ajiri ya kuboresha kilimo cha pamba katika maeneo yao.
Vikundi hivyo ambavyo hujishughulisha na kilimo cha pamba vimepokea hundi hiyo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, wakati wa uzinduzi wa msimu wa kilimo wa mwaka 2017/2018.
Akizindua msimu wa kilimo na kukabidhi hundi kwa vikundi hivyo Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt Seif Shekalage alisema halmashauri imetekeleza sera ya kuwawezesha vijana na wanawake kwa kuwajengea uwezo katika kujiletea maendeleo ya kujikomboa na umaskini.
Alisema halmashauri imefanikiwa kutekeleza sera hiyo ya kutoa asilimia 5 kwa wanawake na 5 kwa vijana ili kuhakikisha wanajenga uchumi na kipato cha kila mwananchi wa Wilaya hiyo.
Dk Shekalage aliongeza kuwa akinamama na vijana wanapaswa kutambua matumizi sahihi na makusudio ya mkopo waliopokea ili uweze kuwanufaisha katika shughuli zao za kilimo.
Aidha kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Maswa Roggers Limo alisema kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita 2013/2014 hadi 2016/2017 Wilaya yao ilitoa mkopo wa kiasi cha shilingi Mil 75,955,000 kwa vikundi vya wanawake na shilingi 105,182,500 kwa vikundi vya vijana ambapo Milioni 30,162 ,500 ni mapato ya ndani ya Halmashauri.
Hata hivyo Afisa kilimo wa Wilaya hiyo Christopher Simwimba alivitaka vikundi hivyo kutumia mkopo huo ipasavyo na kuhakikisha kabla ya kuanza kupanda katika mashamba yao ni lazima waondoe mazalia ya pamba yaliyokuwa yamebaki ili yasije kuharibu pamba mpya itakayopandwa.
Simwimbi pia aliwasihi wakulima hao kupitia vikundi vyao kutumia mbolea ya samadi ili kurutubisha udongo wa mashamba yao sambamba na kupanda kitaalamu wa kuzingatia sentimeta 90 hadi 40 kwa kila mstari .
Nao baadhi wa wanakikundi vya vikundi hivyo wameishukuru Halmashauri hiyo kwa jitihada wanazozifanya za kuhakikisha wanainua na kufufua kilimo cha zao la pamba ambalo limeonekana kushuka kwa kiwango cha uzalishaji.
Haji Mwarabu mwanakikundi kutoka katika kikundi cha Huruma katika kata ya Mataba aliihakikishia Halmashauri hiyo kupitia Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri yao Dkt Fredrick Sagamiko kuwa watautumia vizuri mkopo huo ili waweze kubadilisha maisha yao kupitia kilimo cha pamba.
Baadhi ya wanavikundi vya vijana na wanawake Wilayani Maswa ,watendaji wa Halmashauri na Baadhi ya madiwani wakiwa katika uzinduzi wa msimu wa Kilimo mwaka 2017/2018 na utoaji wa hundi ya shilingi Milioni 50 kwa vikundi vya wanawake na vijana .
Mkuu wa Wilaya ya Maswa Maswa Dkt Seif Shekalage akimkabidhi mbegu za pamba aina ya YKM08 mwanakikundi cha mama na mtoto ni familia kutoka katika kata ya Kadeto Veronica Seloli wakati wa uzinduzi wa msimu wa kilimowilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa Maswa Dkt Seif Shekalage (KATIKATI) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Mhe.Lucas Mwaniyuki ,pamoja na baadhi ya madiwani wa halmashauri ya maswa mara baada ya makabidhiano ya hundi ya Milioni 50 kwa vikundi 16 vya wanawake na vijana vinavyojihusisha na kilimo.
Bariadi - Somanda
Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.
Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054
Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054
Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz
Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa