• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Dkt Bana Aomba Wizara ya Fedha Kuwezesha Ujenzi wa Mabweni IFM Kampasi ya Simiyu

Posted on: November 22nd, 2019

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Balozi Dkt. Benson Bana ameiomba Wizara ya Fedha na Mipango kuwezesha ujenzi wa mabweni kwa wanafunzi  takribani 500 wanaotarajiwa kudahiliwa mwezi Machi, 2020 katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo hicho Mkoani Simiyu, ili kuwaondolea adha ya kupanga mitaani.

Dkt. Bana ametoa ombi hilo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji alipofanya ziara Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo  kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu.

Dkt. Bana amesema kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaoomba udahili wa masomo, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), kimeanzisha Kampasi ya Kanda ya Ziwa iliyopo Kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi Simiyu, ambapo mwezi Machi 2020 wanafunzi takribani 1000 wanatarajiwa kuanza masomo.

“Ili tuweze kufikia malengo yetu tunaomba mabweni ya kuhimili angalau wanafunzi 500 tu, Mhe. Naibu Waziri tunaomba kuwezeshwa kujenga mabweni haya mengine utuachie tutafanya, tusipofanikiwa hili Mhe. Naibu Waziri, juhudi za Mhe. Mkuu wa Mkoa na viongozi wenzake zinaweza kuishai mahali ambapo si pazuri,” alisema Dkt. Bana.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji amesema Serikali inatambua juhudi za Mkoa wa Simiyu katika elimu na kuahidi kujenga mabweni yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 500 kama alivyoomba Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, ili wanafunzi watakaodahiliwa wapate malazi hususani wanafunzi wa kike.

“Hizi changamoto mlizozitaja na hasa hili la mabweni kwa ajili ya watoto wetu linafanyiwa kazi kwa haraka na ujenzi wa mabweni ya watoto 500 mpaka tutakapofika mwezi Machi inawezekana,” alisema Dkt.  Kijaji.

Naye Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameushukuru uongozi wa Chuo cha IFM kwa uamuzi wa kujenga Kampasi mpya Simiyu na kuamua kuifungua mwaka 2020 ambapo amesema kuwepo kwa chuo hicho kutachangia kuongeza mwamko wa elimu katika mkoa wa Simiyu, huku akiwaalika wawekezaji kuwekeza katika huduma mbalimbali katika kampasi hiyo.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof.Tadeo Satta amewashukuru viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa namna walivyowezesha kupata eneo la ujenzi lenye ukubwa wa ekari 30 ambalo lilitolewa bure na pia walivyosaidia katika hatua ya ujenzi ambapo wametoa wataalam kusaidia kusimamia ujenzi na kupelekea ujenzi kwenda kwa kasi.

Ameongeza kuwa majengo yanayotarajiwa kujengwa katika kampasi ya Simiyu ni jengo la utawala, maktaba, madarasa, maabara ya kompyuta, hosteli za wanafunzi, nyumba za wafanya kazi, kafteria na holi kwa ajili ya mikutano; ambapo kwa awamu ya kwanza ujenzi ulianza mwezi Julai 2019 mpaka sasa jengo la utawala lenye ghorofa moja limefikia asilimia 62 na madarasa yamefikia asilimia 92.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/11/dkt-bana-aomba-wizara-ya-fedha.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa