• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

DC Bariadi: Wadau wa Afya Endeleeni Kuchangia Vitendea Kazi, Miundombinu Kuboresha Huduma za Afya Simiyu

Posted on: July 12th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amewaomba wadau wa afya waliopo mkoani Simiyu kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya  kwa kutenga bajeti kwa ajili ya kuchangia ununuzi wa vitendea kazi na  kujenga miundombinu ya afya.

Kiswaga amevitaja vitendea kazi hivyo kuwa ni pamoja na magari ya kubebea wagonjwa (ambulance), vifaa vya kwenye vituo vya afya ,zahanati na hospitali ili huduma ziendelee kutolewa kwa ufanisi mkubwa.

Ameyasema hayo katika kikao cha wadau wa afya kilichofanyika Mjini Bariadi wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwenye kikao cha wadau wa afya kilichofanyika Julai 11 na Julai 12, 2019 kwenye ukumbi wa kanisa Katoliki mjini Bariadi.

Aidha ameongeza kuwa kuna kila sababu ya mashirika hayo kuongeza majengo na magari ili huduma za afya zizidi kuimarika mkoani hapo.

Pamoja na hayo amesema kuwa kama mkoa watahakikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha kwa wadau wa afya mkoani hapo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

"kila shirika lililopo mkoani hapa linafanya kazi nzuri endeleeni kuzidisha juhudi hizo  bado tuna upungufu wa vitendea kazi , tunaomba muendelee kutafuta fedha huko ili kuhakikisha kwamba vitendea kazi kama magari, magari ya kubebea wagonjwa lakini pia majengo bado ni changamoto pamoja na kazi kubwa nzuri ambazo mmezifanya tunaombeni muendelee kuweka bajeti hizo "alisema Kiswaga na kuongeza kuwa:

“kama mkoa tutahakikisha mashirika haya yanatekeleza majukumu yake bila wasiwasi wowote , watendaji kuanzia ngazi za chini sitegemei kusikia shirika limeshindwa kutekeleza shughuli zake eti kisa mtendaji kakwamisha , watendaji kuanzia ngazi ya chini hakikisheni mnatoa ushirikiano wa kutosha ili mashirika haya yatekeleze majukumu yake”aliongeza Kiswaga

Kwa upande wake Mwenyekiti wa wadau wa afya mkoani hapa Dkt Amiri Batenga ambaye ni mwakilishi wa shirika la umoja wa kimataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani UNFPA mkoa wa Simiyu amesema kuwa wameendelea kuboresha vituo vya kutolea huduma za afya lengo likiwa kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto wachanga.

Aidha, Dkt. Batenga ameongeza kuwa wameshatumia kiasi cha bilioni tano na nusu kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa majengo ,vifaa pamoja na magari mkoani Simiyu huku akiomba Serikali kuendele kusimamia na kuhakikisha vituo na vifaa hivyo vinafanya kazi iliyokusudiwa na wananchi waone haja ya kutumia vituo hivyo maana vimejwngwa kwa ajili yao.

“kujenga vituo vya afya ,kuweka vifaa na kufundisha watumishi ni jambo jingine vituo hivi vinatakiwa vitumike kina mama wajawazito wasipotumia hivi vituo yale malengo hayawezi fikiwa …pale tumejenga vituo 38 nasasa hivi tumeongeza vingine viwili ili kufikia malengo lazima mama aje pale tukiunganisha nguvu ya pamoja kina mama wakafika kwenye vituo vya afya vifo vitaisha kabisa” alisema Batenga

Mkoa wa Simiyu una zaidi ya mashirika 17 yanayofanya kazi bega kwa bega na mkoa yakiwa na lengo la kuunga mkono juhudi za serikali katika sekta mbalimbali ikiwemo afya na elimu.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/07/dc-bariadi-wadau-wa-afya-endeleeni.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa