• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Chama Kikuu cha Ushirika Simiyu Kimetenga shilingi Milioni 36.7 Kusaidia Jamii

Posted on: June 4th, 2020

Chama kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Simiyu(SIMCU) kimetenga jumla ya shilingi milioni 36.7 kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo elimu na afya katika Mkoa wa Simiyu.

Hayo yamesemwa na makamu mwenyekiti wa SIMCU, Bw. Emmanuel Mwerere Juni 04, 2020 Mjini Bariadi  wakati akikabidhi fedha na baiskeli kwa mtoto Ritha Elias (08)  mwenye ulemavu wa miguu.

“Chama kikuu cha ushirika mkoa wa Simiyu kimetenga jumla ya shilingi 36,700,000/= kati ya hizo shilingi 24,000,000/= itasaidia elimu kwa watoto wenye ulemavu shilingi 12,000,000/= tutanunua mashuka kwa ajili ya Hospitali zote za mkoa wa Simiyu na shilingi 700,000/= kwa ajili ya kumsaidia mtoto Ritha Elias ambaye ni mlemavu wa miguu,”alisema Mwerere.

“SIMCU leo tunamkabidhi mtoto Ritha Elias kiasi cha shilingi 300,000/=  ikiwa ni ada ya shule na nauli ya kwenda na kurudi na baiskeli yenye thamani ya shilingi 400,000/= ambayo itamsaidia akiwa nyumbani na shuleni, "aliongeza Mwerere.

Aidha, Mwerere ameongeza kuwa mpango huo ni mwendelezo wa shughuli za chama hicho katika kusaidia jamii huku akiongeza kuwa awali walitoa zaidi ya shilingi milioni 3 kwa ajili ya chakula cha wanafunzi waliokuwa kwenye kambi za kitaaluma.

Katika hatua nyingine Mwerere ameomba makampuni ya pamba yaliyonunua pamba msimu wa wa mwaka 2018/2019 kulipa fedha za ushuru kiasi cha shilingi milioni 729,520,255.

Awali akiongea kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga ameipongeza SIMCU kwa kutenga fedha hizo na kurudisha shukrani kwa jamii ikiwemo kumsaidia mtoto mwenye ulemavu wa miguu.

‘’Baadhi ya vyama vya ushirika vinafanya vizuri lakini fedha zao zinaishia kwenye posho na vikao, niwapongeze kwa kutenga kiasi cha milioni 36.7 kwa ajili ya huduma za kijamii ,leo mmekabidhi baiskeli kwa mtoto huyu mwenye ulemavu na mmemwingiza katika mpango wa kumsomesha mpaka mwisho wa masomo yake niwapongeze sana na kingine huyu binti ana kipaji cha kuchora ni mchoraji mzuri sana ’’ alisema Kiswaga.

Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Simiyu, Ibrahimu Kadudu amesema kurudisha kwa jamii sehemu ya faida ambayo vyama vya ushirika vinapata  huo ndio umuhimu wa ushirika, ambapo amebainisha kuwa pamoja na kutenga fedha kwa ajili ya elimu na afya,  awali SIMCU ilichangia fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya janga la CORONA.

Kwa upande wake bibi wa mtoto wa Ritha Elias, Perpetua Mtaima amesema mtoto huyo alizaliwa akiwa hana miguu yote miwili huku akiongeza kuwa pamoja na ulemavu huo mtoto huyo ana uelewa wa vitu vingi japokuwa ni mdogo na kwa hivi sasa anasoma darasa la tatu katika shule ya watoto wenye ulemavu ya Jeshi la Wokovu iliyopo jijini Dar es salaam na amekuwa akifanya vizuri darasani.

“Nilikuwa naomba msaada kwa watu mbalimbali akiwemo Mkuu wa wilaya ili mtoto huyu apate elimu na hana miguu nikushukuru sana baba (mkuu wa wilaya ) na mjukuu wangu huyu amekuwa akiniambia siku moja atanibeba kwenye gari lake pia atanipeleka ofisini kwake na akimaliza masomo atapata kazi…nawashukuru wote mlionisaidia kunipatia nauli ya kumpeleka Dar es Salaam’’ alisema Perpetua.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:- https://simiyuregion.blogspot.com/2020/06/chama-kikuu-cha-ushirika-simiyu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa