• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

AMREF Watoa Gari la Wagonjwa Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu

Posted on: May 11th, 2018

 Shirika lisilo la kiserikali la AMREF limetoa msaada wa gari la kubebea wagonjwa lenye thamani ya shilingi milioni 150 katika Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu ambalo
 litatumika kuharakisha rufaa za wagonjwa hususani wakinamama wajawazito na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi Mkoani humo. .

 Akikabidhi gari hilo kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka,Meneja wa AMREF wa program wa Afya ya mama na Mtoto Tanzania Dr.Sarafina Mkuwa amesema kuwa Shirika hilo kupitia Mradi wa Uzazi Uzima umetambua umuhimu wa kutatua changamoto katika sekta ya afya na kutoa gari hilo ili kunusuru vifo vya akinamama na watoto Mkoani Simiyu.

“Hii ‘ambulance’itasaidia wagonjwa watakaohitaji huduma za rufaa kwa haraka, Mkuu wa Mkoa nakukabidhi ambulance hii ili iweze kuusaidia mkoa katika kuhakikisha kwamba wakina mama wa Mkoa wa Simiyu wanajifungua salama na wanapata huduma zote za rufaa kwa haraka” alisisitiza Dkt. Mkuwa.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameishukuru AMREF kwa kutoa gari hilo ambapo amesema msaada huo umejibu hoja ya Mkoa huo waliyokubaliana na wadau wa afya kuwa fedha za wadau hao zinapaswa kujibu mahitaji ya wananchi katika sekta ya afya, ikiwa ni pamoja na vitendea kazi kama magari na kujenga miundombinu ya afya badala ya kuzielekeza zaidi kwenye semina.

Aidha, amesema gari hilo litakuwa msaada mkubwa kwa Hospitali Teule ya mkoa ambayo hapo awali ilikuwa ikiilazimu kuazima magari kutoka katika hospitali na vituo vingine vya afya pale huduma za haraka zinapohitajika kwa ajili ya kuwasafirisha wagonjwa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Bugando.

“Tunawashukuru sana AMREF kwa msaada huu, gari hili litatusaidia sana kwenye hospitali yetu maana walikuwa wakipata dharura ‘ambulance’ inaitwa kutoka kwenye maeneo mengine, jana Mhe.Esther Midimu Mbunge wa Viti Maalum (CCM) aliuliza ni lini Hospitali ya Mkoa wa Simiyu itapata gari la wagonjwa  leo AMREF wamejibu swali lake” alisema Mtaka

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa huyo amewahakikishia viongozi wa AMREF kuwa Serikali mkoani humo itaendelea kushirikiana nao katika masuala mbalimbali ya kuboresha huduma za afya na kutatua changamoto za sekta ya Afya kwa wananchi wa Mkoa wa Simiyu.


 Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali Teule ya Mkoa,Dkt. Fredrick Mlekwa amesema wanalishukuru shirika la Amref kwa msaada huo kwani hapo awali walikuwa wakipata shida kuazima gari hilo katika wilaya zingine za Mkoa na akaahidi kuwa Hopsitali hiyo italitunza gari hilo na kulitumia kwa lengo lililokusudiwa..

 Mwisho

KUPATA PICHA ZAIDI JUU YA HAFLA YA MAKABIDHIANO YA GARI HILI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/05/amref-watoa-gari-ya-wagonjwa-hospitali.html

 

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa