• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri Mwijage: Serikali Inaendelea Kujenga Uchumi Imara, Shindani

Posted on: October 28th, 2018

Waziri wa viwanda,biashara na uwekezaji Mhe. Charles Mwijage amesema serikali inaendelea kujenga uchumi wa Kitaifa(jumuishi) ulio imara na wenye ushindani kuelekea uchumi wa kati ifikapo 2025 kwa kuanzia uzalishaji mashambani hadi sokoni.

Hayo ameyasema wakati akihitimisha Maonesho ya (SIDO) Kitaifa yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu, yakiwa na Kauli Mbiu: “PAMOJA TUJENGE VIWANDA KUFIKIA UCHUMI WA KATI”

Mhe. Mwijage amezitaja baadhi ya sifa za uchumi wa Kitaifa (Jumuishi) kuwa ni pamoja na Kipato cha wastani kwa Mtanzania kufikia dola 3000 kwa mwaka ifikapo 2025, Watanzania kuwa na maisha mazuri, watu kuwa na elimu na wepewi kwa kujifunza, pamoja na kuwa na uchumi imara ulio shindani.

“Tunataka mwaka 2025 tuwe na uchumi imara na shindani lakini tuendelee kudumisha amani na msihikamano; njia rahisi ya kufikia mahali mbapo kipato cha wastani cha Mtanzania kuwa dola 3000 kwa mwaka ni kupitia uchumi wa viwanda na uchumi wa viwanda ni zaidi ya viwanda, uchumi wa viwanda unaanzia shambani hadi sokoni” alisema.

Katika hatua nyingine alitoa wito kwa Watanzania kulinda viwanda vya ndani hapa nchini kwa kununua bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Mhe. Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Mapinduzi ya viwanda yanatokana na Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO), hivyo ni vema wizara ya viwanda ,biashara na uwekezaji ikaliwezesha shirika la kuhudumia viwanda vidogo ili kutekeleza azma ya Tanzania ya viwanda.

Akizungumzia maonesho ya Viwanda vidogo Mkurugenzi Mkuu wa SIDO Prof. Silvester Mpanduji, amesema jumla ya wajasiriamali 515 kutoka mikoa 23 nchini na nchi jirani za Uganda na Burundi, wameshiriki manesho haya na kupata fursa ya kuonesha bidhaa wanazozalisha na kubadilisha uzoefu katika masuala mbalimbali.

Aidha, amesema kupitia maonesho hayo mashine za kuongeza thamani katika mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi na misitu zenye thamani ya zaidi ya shilingi 800 zimenunuliwa na nyingine kuwekewa ahadi ya kununuliwa.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa UNDP anayeshughulikia miradi Amoni Manyama ameahidi kuwa Shirika hilo liko tayari kushirikiana na Serikali hapa nchini katika Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda kwa kutoa msaada wa kifedha na utaalam wa kuchambua miradi ya viwanda katika Mkoa wa Simiyu na mikoa mingine pia.

Maonesho ya Viwanda Vidogo SIDO Kitaifa yaliyofanyika kwa muda wa siku sita katika Viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu yalifunguliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Oktoba 23, 2018, pamoja na wajasirimali 515 kushiriki takribani taasisi za Umma na Binafsi 24 zimeshiriki maonesho haya.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/10/mwijage-viwanda-vidogo-biashara-ndogo.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa