• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aiagiza Mikoa Minane Inayolima Pamba Kuongeza Kasi ya Usimamizi kwa Kutoa Elimu, Simiyu Yaahidi Kuongeza Uzalishaji hadi Kufikia Tani 240,000.

Posted on: January 18th, 2019

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza wakuu wa mikoa minane inayolima pamba kwa wingi nchini ikiongozwa na mkoa wa Simiyu kusimamia kikamilifu uzalishaji wa zao hilo katika msimu huu na kuhakikisha wakulima wanapewa elimu stahiki itakayowawezesha  kuongeza tija katika kilimo cha zao hilo.

Waziri Mkuu Majaliwa ametoa kauli hiyo katika mkutano uliomwezesha kuwasiliana moja kwa moja kwa njia ya video (Video conference) na wakuu wa mikoa ya Simiyu, Mara, Shinyanga, Geita, Kagera,  Mwanza,  Tabora na Singida na kusema kuwa msimu huu hatarajii kuona changamoto zilizoshusha kiwango cha uzalishaji katika msimu uliopita zinajirudia huku akimwagiza  mkurugenzi mkuu wa bodi ya pamba nchini kuhakikisha dawa za kuua wadudu zinawafikia wakulima kwa wakati.

“ Mwaka huu lengo letu ni kuzalisha tani laki sita, ninaamini hili linawezekana endapo  ninyi waheshimiwa wakuu wa mikoa mtalisimamia jambo hili kikamilifu, nendeni mkahakikishe maafisa ugani pamoja maafisa ushirika wanatoka ofisini na kuwatembelea wakulima katika maeneo yao na kuwaelimisha kuhusu namna ya kupata mitaji pamoja na uwezekano wa  kupata soko la uhakika baada ya mavuno”.

“Tukiwa bado katika ngazi ya mkoa, pia hakikisheni mnawasimamia Makatibu tawala wanaoshughulikia kilimo pamoja mrajisi wafuatilie mara kwa mara kujiridhisha kama agizo hili linatekelezwa kwa vitendo”, alisisitiza Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha Waziri Mkuu Majaliwa ameagiza mikoa ipitie upya utaratibu unaotumika hivi sasa unaoruhusu fedha yote inayokusanywa kupelekwa kwenye miradi ya maendeleo na badala yake uanzishwe utaratibu mpya utakaoruhusu  sehemu ya makusanyo hayo kutumika kuboresha kilimo cha pamba.

Akijibu swali laWaziri Mkuu Majaliwa kuhusu utaratibu unaoweza kumsaidia mkulima kuondokana na dhana ya utegemezi wa mikopo, Mkuu wa mkoa wa Simiyu mkoa ambao ndiye mzalishaji mkuu wa pamba nchini kwa 55% Anthony Mtaka amesema, njia pekee itakayowasidia wakulima kuondokana na hali hiyo ni bodi ya pamba kutochukua sehemu ya mapato ya shilingi 100 kwa kila kilo kama ambavyo imekuwa ikifanya badala yake fedha hizo zibaki kwenye AMCOS kama njia ya kuimarisha kilimo cha zao hilo.

“ Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa upande wetu Simiyu msimu huu pekee tunatarajia kuvuna kilo milioni 240, na kama bodi ya pamba watachukua kiasi cha shilingi 100 kwa kila kilo kama ambavyo wamekuwa wakifanya maana yake watachukua shilingi bilioni 24, ambazo kama zikibaki kwenye AMCOS si haba,  ndio maana tunasisitiza ipo haja ya kuutazama upya mfumo huu na endapo sote tutaafiki kuufanyia mabadiliko, Simiyu tupo tayari kuwa wa kwanza kulitekeleza na tutaanza na wilaya mojawapo tuone kama una tija”, aliongeza Mhe Mtaka.

Huu ni mkutano wa kwanza wa aina hii kati ya waziri mkuu na wakuu wa mikoa ambapo ameiagiza kampuni ya simu TTCL kuhakikisha mifumo yote inayoruhusu mawasiliano ya moja kwa moja kwa njia ya video inafanya kazi katika ofisi zote za wakuu wa mikoa nchini  ambapo hivi karibuni kwa mara nyingine anatarajiwa kufanya mkutano kama huu na wakuu wa mikoa 4 inayolima chai kwa wingi nchini ikiwemo Tanga, Iringa, Njombe na Mbeya.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2020 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 07, 2019
  • Matokeo ya Kidato cha NNe mwaka 2018 January 24, 2019
  • Fungua

Habari Mpya

  • Kila Mtumishi Itilima Ashiriki Kikamilifu Ukusanyaji Wa Mapato: RAS Simiyu

    February 27, 2021
  • RAS Simiyu Awaasa Viongozi wa Dini, Waganga wa Tiba Asili Kushiriki Kupunguza Vifo vya Wajawazito na Watoto

    February 27, 2021
  • Watu Wenye Ulemavu Watakiwa Kuchangamkia Fursa ya Mikopo ya Asilimia Mbili Kutoka Halmashauri

    January 30, 2021
  • RC Simiyu Asitisha Leseni Za Uchimbaji Madini Mgodi wa Lubaga

    December 17, 2020
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa