• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Simiyu Aagiza Maafisa Utamaduni, Maafisa Maliasili Kutambua Vikundi Vya Utamaduni vinavyocheza Ngoma na Wanyama ili Vitafutiwe Vibali

Posted on: July 9th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka  amewaagiza Maafisa Utamaduni na Maafisa Maliasili wa Halmashauri zote mkoani humo kutambua vikundi vya Utamaduni vuinavyocheza ngoma zao na wanyama hai kama nyoka aina ya chatu na fisi ili viweze kuwekewa utaratibu wa kupata vibali vya Serikali.

Mtaka ameyasema hayo Julai 08, 2018 wakati akizungumza na wananchi katika  Tamasha la SIMIYU JAMBO FESTIVAL Mjini Bariadi, ambalo limehusisha mashindano ya ngoma za asili (Wagika na Wagalu), mbio za baiskeli(Kilomita 150 wanaume na kilomita 100 wanawake), mbio fupi(Kilomita 10 na Kilometa tano), uandishi wa insha, likiwa limeshirikisha washiriki kutoka  mikoa mbalimbali hapa nchini, nchi jirani ya Kenya.

Mtaka amesema yuko tayari kuwasaidia wanautamaduni hao ambao wanacheza ngoma zao na wanyama walio hai kulipia gharama zote za kupata vibali hivyo, ili waendelee kuutambuisha na tangaza utamaduni wa mkoa huo duniani.

“Nawaagiza maafisa Utamaduni na Maliasili wote kwenye halmashauri za Mkoa wa Simiyu wavitambue vikundi vyote vya utamaduni vinavyocheza na chatu, fisi na mtoe utaratibu wa kupata vibali vya kuwatumia wanyama hao, kama ni malipo mimi kama Mkuu wa Mkoa niko tayari kuwasaidia hao watu kulipa ili wawe kwenye utaratibu wa serikali” alisema Mtaka.

Kwa upande wake Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Tulia Ackson ambaye alikuwa mageni Rasmi katika Simiyu Jambo Festival amesema suala la wanautamaduni kucheza na wanyama hai lipo maeneo mengi hapa nchini , hivyo akasisitiza kuwa ni vema suala la utaratibu wa kutoa vibali ukapatiwa ufumbuzi waweze kupewa vibali kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa ili kuwapa uhuru kufanya kazi zao.

“Hili jambo linapaswa kufanyiwa kazi,  kama nilivyowaambia awali kuwa wenzetu wa Bujora Mwanza walipata fursa ya kwenda India kuonesha kazi zao za utamaduni na ngoma ya asili ambayo huwa wanacheza na nyoka lakini hawakufanikiwa kusafiri na nyoka kwa sababu ya changamoto ya kibali” alisema.

Tamasha la Simiyu Jambo Festival mwaka 2018 lilishirikisha washiriki kutoka mikoa 13 hapa nchini na nchi jirani ya Kenya huku likihusisha mashindano ya mbio za baiskeli (kilomita 150 wanaume, kilomita 100 wanawake, kilomita 10 walemavu), mashindano ya mbio fupi(kilomita 10 na kilomita tano), mashindano ya ngoma za asili(Wagika na Wagalu) na mashindano ya uandishi wa insha kwa wanafunzi wa shule za sekondari.

Bw. Mayunga Kidoyayi akionesha umahiri wake wa kucheza na manyama fisi wakati wa Tamasha la SIMIYU JAMBO FESTIVAL Mjini Bariadi, ambalo limehusisha mashindano ya ngoma za asili (Wagika na Wagalu), mbio za baiskeli(Kilomita 150 wanaume na kilomita 100 wanawake), mbio fupi(Kilomita 10 na Kilometa tano), uandishi wa insha, likiwa limeshirikisha washiriki kutoka  mikoa mbalimbali hapa nchini, nchi jirani ya Kenya.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2020 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 07, 2019
  • Matokeo ya Kidato cha NNe mwaka 2018 January 24, 2019
  • Fungua

Habari Mpya

  • RC Simiyu Asitisha Leseni Za Uchimbaji Madini Mgodi wa Lubaga

    December 17, 2020
  • Waziri wa Kilimo Prof. Mkenda, Naibu Waziri TAMISEMI Dkt Dugange Wanogesha RCC Simiyu

    December 16, 2020
  • TANROADS Simiyu Kutumia Bilioni 11.4 Ujenzi wa Barabara na Madaraja

    December 16, 2020
  • Viongozi, Wananchi na Wadau Simiyu Watakiwa Kushirikiana Kukamilisha Ujenzi wa Madarasa

    December 13, 2020
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa