• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Apongeza Geita kwa Ubunifu Kufanya Maonesho ya Kipekee ya Dhahabu Nchini

Posted on: September 28th, 2018

Na Stella Kalinga, Simiyu

Mkuu wa Mkoa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewapongeza viongozi wa Mkoa wa Geita wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhandisi. Robert  Gabriel kwa ubunifu waliofanya wa kufanya Maonesho ya Kipekee ya Tekonolojia bora ya dhahabu hapa nchini.

Mtaka ameyasema hayo mara baada ya kuzungumza na viongozi wa Mkoa wa Geita na kutembelea mabanda ya maonesho katika Maonesho ya Teknolojia ya Dhahabu yanayofanyika  Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita kuanzia Septemba 24, 2018.

Amesema Watanzania wengi wamekuwa wakienda kushiriki maonesho ya dhahabu katika mataifa mbalimbali barani Afrika na nje ya bara la Afrika lakini kupitia maonesho haya Watanzania wameanza kujionea teknolojia mbalimbali za uchimbaji wa madini hapa nchini.

“ Ninawapongeza sana viongozi wa Geita kwa kuandaa maonesho haya ya kipekee hapa nchini, tumekuwa na shughuli nyingi sana za uchimbaji madini lakini sisi sote ni mashahidi shughuli hizi tumekuwa tukiziona wakati wa Mei Mosi kupitia kile chama kinachohusisha watu wanaofanya kazi za madini, hatujapata jambo linaloonesha shughuli za migodini na mazao yanayotokana na migodi kama dhahabu” alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa ubunifu huo uliofanywa na Viongozi wa Mkoa wa Geita hasa wa kuyapa maonesho haya jina la Kiswahili ya “Maonesho ya Dhahabu” ambalo linasadifu shughuli zinazofanyika katika mkoa huo ambao ni mzalishaji mkubwa wa dhahabu, utachangia kuongeza watalii na wageni wengi watakaokuja hapa nchini kupitia maonesho hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi. Robert Gabriel ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kushuhudia maonesho hayo ili kujionea teknolojia za uchimbaji madini, kupata huduma za kifedha katika taasisi za kifedha, kupata huduma na elimu juu ya utatuzi wa changamoto za kibiashara hususani upatikanaji wa mitaji na changamoto za uchimbaji katika kliniki ya biashara.

Aidha, Mhandisi. Gabriel amesema maendeleo katika mkoa wa Geita hayaepukiki kutokana na sekta ya madini kuwa na  mchango mkubwa katika uchumi ambapo amebainisha kuwa kupitia uchimbaji dhahabu mkoa unapata ushuru, fedha za msaada kwa jamii (Corporate  Social Responsibility) kutoka kwenye makampuni yanajihusisha na uchimbaji madini zilizosaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Mhe. Leonald Bugomola amesema maonesho ya dhahabu mwaka 2019 yataanza mapema na Halmashauri yake kama mwenyeji wa maonyesho hayo imejipanga kutafuta eneo kubwa zaidi ekari 100 ,  kwa kuwa mpango wa mkoa ni kuwa na maonesho yenye hadhi ya Kimataifa yatakoshirikisha washiriki wengi ikilinganishwa na mwaka huu.

Nao baadhi ya wachimbaji wadogo wameshukuru uanzishwaji wa maonesho hayo ambayo yatasaidia kupata utaalamu juu teknolojia mbalimbali zinazotumika kuchimba madini na kupata elimu ya namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali katika sekta ya madini kutokana na wadau mbalimbali kukutanishwa pamoja na kujadiliana kuhusu maendeleo ya sekta ya madini.

Maonesho ya Tekonolojia Bora Dhahabu mkoani Geita yameanza Septemba 24, 2018 na yanatarajiwa kuhitimishwa Septemba 30, 2018 yakiwa na Kauli Mbiu: TEKNOLIJIA BORA YA UZALISHAJI WA DHAHABU KWA MAENDELEO YA KIJAMII NA UCHUMI WA VIWANDA”

MWISHO.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2020 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 07, 2019
  • Matokeo ya Kidato cha NNe mwaka 2018 January 24, 2019
  • Fungua

Habari Mpya

  • Kila Mtumishi Itilima Ashiriki Kikamilifu Ukusanyaji Wa Mapato: RAS Simiyu

    February 27, 2021
  • RAS Simiyu Awaasa Viongozi wa Dini, Waganga wa Tiba Asili Kushiriki Kupunguza Vifo vya Wajawazito na Watoto

    February 27, 2021
  • Watu Wenye Ulemavu Watakiwa Kuchangamkia Fursa ya Mikopo ya Asilimia Mbili Kutoka Halmashauri

    January 30, 2021
  • RC Simiyu Asitisha Leseni Za Uchimbaji Madini Mgodi wa Lubaga

    December 17, 2020
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa