• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Maafisa Tarafa Simiyu Wakabidhiwa Pikipiki Utekelezaji Ahadi ya Rais Magufuli

Posted on: May 8th, 2020

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amewakabidhi pikipiki Maafisa Tarafa 15 wa Mkoa huo ambazo ni utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa mwezi Mei 2019 wakati alipokutana na Maafisa tarafa wote nchini katika kikao kazi jijini Dar es Salaam.

Akiwakabidhi pikipiki hizo Mei 08, 2020 Mjini Bariadi Sagini amemshukuru Mhe. Rais kwa kutoa pikipiki hizo zitakazorahisisha utekelezaji wa majukumu ya Maafisa tarafa huku akiwaagiza kuzitunza na kuzitumia kwa malengo yaliyokusudiwa; ikiwa ni pamoja na kufuatilia mkakati wa elimu wa Mkoa wa kuwawezesha wanafunzi kusoma wakiwa katika likizo ya dharura ya tahadhari ya maambukizi ya Virusi vya Corona.

Tumeandaa mkakati  wa mkoa wa kuwawezesha wanafunzi kusoma kipindi ambacho wako likizo ikiwa ni tahadhari ya maambukizi ya Virusi vya Corona; moja ya majukumu yenu katika kipindi hiki ni kuhakikisha mkakati unatekelezwa kwenye maeneo yenu ya utawala; walimu, maafisa elimu watatimiza wajibu wao nanyi pia mna sehemu yenu,”alisema Sagini.

Aidha, Sagini amewataka maafisa tarafa hao kuzitumia pikipiki hizi kwa kuwafikia wananchi wote wakiwemo wakulima hasa kipindi hiki cha mavuno na lengo kuu likiwa ni kuwaasa kutunza chakula.

Awali akisoma taarifa katibu tawala msaidizi utawalana rasilimaliwatu katika Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Ekwabi Mujungu amewataka maafisa tarafa hao kuzitumia pikipiki hizo kwa madhumuni yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kusukuma shughuli za maendeleo ya jamii ikiwemo kusimamia miradi ya elimu ,afya kilimo na hifadhi ya mazingira.

Wakati huo huo Mujungu ametoa maelekezo kwa makatibu tawala wa wilaya mkoani Simiyu kutenga fedha kwa ajili ya mafuta na matengenezo ya pikipiki hizo kwa kila tarafa ili pikipiki hizo ziweze kudumu kwa muda mrefu.

Akiongea kwa niaba ya maafisa tarafa mara baada ya kukabidhiwa pikipiki hizo afisa tarafa ya Dutwa , Isabela Nyaulingo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwawezesha kupata usafiri huo ambao utarahisisha utendaji kazi wao huku akiahidi kuwa watazitunza na kufuata maelekezo yote waliyopewa na viongozi.

Jumla ya pikipiki 15 zimekabidhiwa kwa maafisa tarafa mkoani hapa zikiwa na thamani ya shilingi milioni 33,285,000/=, ambapo  pikipiki moja inagharimu kiasi cha shilingi milioni 2,219,000.

Tarafa zilizonufaika mkoani Simiyu ni Dutwa, Nkololo na Muhango(BARIADI), Kivukoni na Busega(BUSEGA), Itilima, Kanadi, Bumela na Kinang'weli (ITILIMA) Mwagala,Sengerema,na Nung'hu( MASWA), Kisesa Nyalanja na Kimali (MEATU).

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:http://simiyuregion.blogspot.com/2020/05/maafisa-tarafa-simiyu-wakabidhiwa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2020 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 07, 2019
  • Matokeo ya Kidato cha NNe mwaka 2018 January 24, 2019
  • Fungua

Habari Mpya

  • Naibu Waziri Silinde Aridhishwa Ujenzi wa Bwalo, Madarasa Sekondari ya Anthony Mtaka Busega

    March 06, 2021
  • A NaibuWaziri Silinde Aridhishwa Ujenzi wa Bwalo, Madarasa Sekondari ya Anthony Mtaka Busega

    March 06, 2021
  • Naibu Waziri Silinde Atoa Miezi Miwili Bariadi, Itilima Kukamilisha Mabweni

    March 05, 2021
  • Bilioni 75 Kujenga Kituo Cha Kupozea Umeme Simiyu

    March 04, 2021
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa