• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Kila Mtumishi Itilima Ashiriki Kikamilifu Ukusanyaji Wa Mapato: RAS Simiyu

Posted on: February 27th, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amewataka watumishi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu kuwa sehemu ya Halmashauri hiyo katika ukusanyaji wa mapato ili Halmashauri hiyo iweze kupanda katika ukusanyaji mapato na  kupata uwezo wa kujiendesha.

Mmbaga ameyasema hayo wakati akizungumza na baadhi ya watumishi wa tarafa ya Kinang’weli wilayani Itilima wakati wa ziara yake yenye lengo la kuwasiliza na kuzungumza na watumishi iliyofanyika jana Februari 26, 2021.

‘Halmashauri yetu haifanyi vizuri katika ukusanyaji wa mapato, kutokana na hali hii ya ukusanyaji baadi ya masuala yenu muhimu kama watumishi mnaweza msiyapate kwa wakati hivyo kila mtumishi ajulikane kama afisa mapato wa halmashauri, hili si jukumu la Mkurugenzi na Mtunza Hazina wa Halmashauri pekee, wote mshirikiane kukusanaya mapato kwa uadilifu,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga amewataka watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima kuwa waangalifu katika matumizi ya mapato yanayokusanywa kwa kuhakikisha wanawekeza katika maeneo yenye tija na matokeo.

Sambamba na hilo Mmbaga amewataka watumishi hao kuziba mianya yote ya ubadhilifu na kumwataka viongozi kuwachukulia hatua watumishi watakaothibitika pasipo shaka kuwa wamefanya ubadhilifu wa mali za umma na katu wasiwafumbie macho.

Kwa upande wao watumishi wa lioshiriki katika kikao hicho walipata fursa fursa ya kuwasilisha changamoto zao ikiwa ni pamoja na kuomba Katibu Tawala wa Mkoa kama Mkuu wa Utumishi wa Umma ndani ya Mkoa aweze kuzipatia ufumbuzi ambazo ni kulipwa stahiki zao ikiwa ni pamoja na malimbikizo ya mishahara, madai ya fedha za kujikimu na nauli kwa watumishi wapya, upandishwaji wa madaraja na suala la uhamisho.

Katika kuyapatia ufumbuzi masuala haya Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amesema ni vema wakuu wa taasisi wapewe taarifa sahihi juu ya upandishwaji wa madaraja na uhamisho wa watumishi ili waweze kuwaelimisha na kuwapa taarifa sahihi za masuala hayo watumishi walio chini yao.

Aidha, Mmbaga amemtaka mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya itilima kuweka mpango mkakati wa kulipa madai mbalimbali ya watumishi ikiwa ni pamoja na nauli na fedha za kujikimu ili waweze kulipwa kulingana na halmashauri itakavyopata fedha.

Naye Afisa Utumishi wa Halmashauri amesema suala la kupandishwa madaraja kwa watumishi walioajiriwa kuanzia mwaka 2014 halijafanyika kwa nchi nzima si kwa Itilima peke yake hivyo amewasihi watumishi hao kuendelea kuwa watulivu mpaka yatakapotolewa maelekezo na Ofisi ya Rais Utumishi juu ya upandishaji wa vyeo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Wilaya ya Itilima, Bi. Elizabeth Gumbo amewataka wakuu wa shule na wakuu wa Vituo vya kutolea huduma za afya wilayani humo kuyawekea mipaka asili maeneo yaliyo chini yao ili kuepusha maeneo hayo kuvamiwa na wananchi ambapo uvamizi huo unaweza kuleta migogoro katika jamii inayozunguka taasisi hizo.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/02/awatakakila-mtumishi-itilima-ashiriki.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2020 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 07, 2019
  • Matokeo ya Kidato cha NNe mwaka 2018 January 24, 2019
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wanafunzi Simiyu Waomba Kambi za Kitaaluma Ziwe Endelevu

    April 14, 2021
  • Wastaafu Wawaasa Watumishi Kufanya Kazi kwa Kujituma

    April 14, 2021
  • Malalamiko ya Wachimbaji, Wenye Mashamba Mgodi wa Bulumbaka Bariadi Yashughulikiwe: RAS Simiyu

    April 08, 2021
  • Viongozi Simiyu Waaswa Kutumia Busara Badala ya Nguvu

    March 14, 2021
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa